MABINGWA NDANI YA DAR NA KOMBE

MABINGWA wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2022/23 Yanga leo Juni 10, 2022 wameandaa paredi la ubingwa wao.

Timu hiyo chini ya Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi ilishuhudia ubao wa Uwanja wa Sokoine ukisoma Tanzania Prisons 0-2 Yanga.

Mabao ya Yanga ni mali ya Fiston Mayele mwenye mabao 17 pamoja na Yannick Bangala ambaye naye alitupia bao ugenini.

Baada ya mchezo huo walikabidhiwa taji la msimu wa 2022/23 na miongoni mwa nyota ambao walikuwa kwenye sherehe hizo ni pamoja na beki Dickson Job, Kibwana Shomary na Aboutwalib Mshery hawa wote kutoka pande za Morogoro.

Ni ubingwa wa pili mfululizo kwa Yanga ya Nabi baada ya kufanya hivyo pia msimu wa 2021/22.

Kibindoni imekusanya pointi 78 baada ya kucheza mechi 30 za ligi.