LEGEND kwenye ulimwengu wa soka ambaye anatajwa kuwa mchezaji bora wa muda woteraia wa Brazil Pele amewaomba mashabiki na wale wanaomfuatilia wasiwe na mashaka kuhusu afya yake.
Nyota huyo kupitia mitandao ya kijamii ameandika ujumbe ambao unaeleza kwamba anaendelea vizuri na matibabu anaamini atarejea kwenye ubora wake.
Pele alipelekwa hospitali ya Sao Paulo tangu Jumanne kutokana na kutokuwa fiti kwa afya.
Nyota huyo amesema:”Ninataka kila mtu ambaye anafuatilia uhusu mimi awe na utulivu, ninaendelea vizuri na ninapewa matibabu mazuri pia.
“Kwa namna ambavyo ninafuata maelekezo na matibabu ambayo ninapata nina amini nitakuwa imara na kurejea kwenye ubora, asante kwa kujali na asanteni sana,”.
Ni tatizo la kansa ambalo inaripotiwa kwamba anasumbuliwa nayo nyota huyo mwenye miaka 82.
Tottenham Hotspur forward Dominic Solanke battles with Crystal Palace defender Maxence Lacroix during the English championship Premier League football match between Crystal Palace and Tottenham Hotspur on 27 October 2024 at Selhurst Park in London, England - Photo Ian Stephen / ProSportsImages / DPPI (Photo by IAN STEPHEN / ProSportsImages / DPPI via AFP)