>

GEITA GOLD BADO WANA MATUMAINI KIMATAIFA

 WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, Geita Gold wamewashukuru mashabiki kwa sapoti yao licha ya kupoteza mchezo wa kwanza kimataifa kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Hilal Al Sahil.

Kocha Mkuu wa Geita Gold, Felix Minziro aliongoza kikosi hicho kwenye mchezo huo na sasa ni mahesabu kuelekea mchezo wa marudio unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Azam Complex, Septemba 17,2022.

Kwa mujibu wa Mathias Wandiba, kocha msaidizi wa Geita Gold aliweka wazi kuwa kila mmoja anakazi kubwa ya kufanya kutafuta ushindi wa timu.

“Bado kazi ipo na kila mchezaji anapenda kupata matokeo, mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi tuna amini kuwa tutafikia malengo yetu,” amesema.