Yanga SC 2-0 Pamba Jiji FC

MABINGWA watetezi wa ligi, Yanga SC wameendeleza ubabe wao mbele ya Pamba Jiji FC kwa kusepa na pointi tatu mazima ndani ya uwanja.

Baada ya dakika 90 Agosti 28, 2026 ilikuwa Yanga SC 2-0 Pamba Jiji FC, Uwanja wa KMC Complex.

Mabao ya Yanga SC yalifungwa na Maxi Nzengeli dakika ya 17 na Ibrahim Toure dakika ya 22 katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa.

Mchezaji bora wa mchezo alichaguliwa kuwa Maxi ambaye amekuwa katika kiwango bora kwenye mechi za mwanzo msimu wa 2026/27.

Unakuwa ni mchezo wa 4, Yanga SC inashinda na Nzengeli anatwaa tuzo yake ya 3 ya mchezaji bora msimu wa 2026/27 alianza kwenye mchezo dhidi ya Namungo FC akatwaa tuzo hiyo mchezo dhidi ya Coastal Union na mchezo dhidi ya Pamba Jiji FC.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, Moyo Wangu Unavuja Damu na Msichana wa Maisha Yangu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Msichana wa Maisha Yangu ni simulizi mpya ambayo inazungumzia nguvu ya ahadi na mabadiliko ya teknolojia ikiwemo matumizi ya AI. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM.

Duniani kote kinapatikana mtandaoni bofya hapa Buy Book: Msichana wa Maisha Yangu by Lunyamadzo Mlyuka on Selar | selar.