Ndala achaguliwa kuwa mwamuzi wa fainali ya AFCON 2025

Jean-Jacques Ndala, mwamuzi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ndiye atakayechukua jukumu la kuongoza mechi ya fainali ya AFCON 2025 kati ya Senegal na Morocco.

Ndala aliwahi pia kuongoza mechi ya ufunguzi ya mashindano hayo kati ya Morocco na Comoros, na ameonyesha uzoefu mkubwa kwenye michuano ya kimataifa.

Seti ya Waamuzi wa Fainali

  • Mwamuzi Mkuu: πŸ‡¨πŸ‡© Jean-Jacques Ndala

  • Wasaidizi: πŸ‡¨πŸ‡© Guylain Ngila & πŸ‡¨πŸ‡© Mwanya Mobilize

  • Mwamuzi wa Nne: πŸ‡ΏπŸ‡¦ Abongile Tom

  • VAR: πŸ‡°πŸ‡² Styven Moyo

Ndala amechezesha mechi nyingi za kimataifa, ikiwemo mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia na mashindano ya CAF Champions League. Mechi ya fainali ya AFCON 2025 itakuwa fainali yake ya nne katika mashindano ya AFCON.