NABI HOI! RAJA CASABLANCA YATWAA UBINGWA WA LIGI KUU MOROCCO

Klabu ya Raja Casablanca imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu Morocco ya Botola Pro bila kupoteza mchezo wowote na inakuwa klabu ya kwanza kihistoria kufanya hivyo na kutwaa ubingwa wa Ligi kwa mara ya 15.

Licha kukaa kileleni mwa msimamo wa Botola Pro kwa wiki 18, FAR Rabat ya Nasreddine Nabi imeshindwa kutwaa ubingwa wa Ligi hiyo huku Raja Casablanca waliokaa kileleni kwa wiki mbili tu wakinyanyua kwapa.

FT: AS FAR 2-0 FUS Rabat

FT: Mouloudia Oujda 0-3 Raja AC

FT: Wydad 1-0 Moghreb Tetouan

1. Raja — Pts 72
2. AS FAR — 71
3. Berkane — 52
4. Union Touarga — 44
5. Olympique de Safi — 44
6. Wydad AC — 44