Home Sports WASHINDI PROMOSHENI YA TWENZETU DUBAI NA PARIMATCH WAPATIKANA

WASHINDI PROMOSHENI YA TWENZETU DUBAI NA PARIMATCH WAPATIKANA

WASHINDI wawili wa promosheni ya Twenzetu Dubai na Parimatch inayoendeshwa na kampuni ya michezo ya kubashiri ya Parimatch wamepatikana na watasafiri Dubai Jumatatu ijayo.

Washindi hao ni Daniel Kasanga, mkazi wa Ruvuma na Mohamed Salim mkazi wa Kinondoni, Dar es Salaam kwa mujibu wa Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Parimatch, Ismail Mohamed.

Ismail amesema kuwa Kasanga ni mshindi wa droo ya wiki ya kwanza na Salim ameshinda droo ya wiki ya pili kupitia mchezo Aviator ndani ya Casino.

Amesema kuwa safari hiyo itagharimiwa na kampuni yao ikiwa pamoja na usafiri, visa, malazi kwenye hoteli ya kifahari na gharama za kutembelea maeneo mbalimbali ya kitalii na kihistoria wakiwa Dubai.

“Kasanga na Salim wameshinda tiketi ya Dubai kupitia mchezo wa Aviator ambao unapatikana kwenye Casino ya Parimatch. Bado kuna nafasi za kushinda safari ya kwenda Dubai pamoja na fedha taslim Sh200,000 kila siku ambazo zinatolewa katika droo ya siku husika. Tunawaomba wadau wetu kuendelea kubashiri na Parimatch ili kuweza kushinda zawadi hizo.” amesema Mohamed.

Kwa upande wake, Kasanga amesema kuwa amefarijika sana kushinda safari hiyo ya kihistoria kwake.

“Pamoja na kuwa na pasi ya kusafiria, sikujua lini nitaitumia pasi hiyo, hivyo kupitia droo ya Twenzetu Dubai na Parimatch, ndoto yangu imefanikiwa,” amesema Kasanga.

Amesema kuwa amefarijika kushinda safari hiyo na pia fedha taslimu Sh500,000 ambazo alizipata chapchap.

Naye Salim amesema kuwa hakuamini mara alipopigiwa simu kuwa ameshinda safari ya Dubai kupitia promosheni ya Parimatch.

“Sikuamini, kwani unawezaje kwenda kutembelea nchi ya kifahari, yenye raha na vivutio mbalimbali kama Dubai kirahisi rahisi tu. Hata hivyo, kupitia aviator, jambo hili limewezekan, nawaambia Watanzania wenye umri kuanzia miaka 18, kubashiri na Parimatch, hawana longolongo.” amesema Salim.

Kampuni ya Parimatch ndio kinara wa michezo ya kubashiri mtandaoni na imekuwa ikitoa ofa kubwa ya bonasi ya Ukaribisho ya 125% hadi kufikia TZs 1,000,000 kwa wateja wapya wanaojiunga nao!

Parimatch imekuwa ikifanya kazi nchini Tanzania tangu mwaka 2019, ikitoa huduma nzuri ikijumuisha malipo ya haraka, odds kubwa na promosheni za kusisimua kwenye soka, Kasino na Michezo ya virtual. Mbali na soka, kampuni ya Parimatch pia hutoa mamia ya matukio kila siku kwenye tenisi, UFC, mpira wa vikapu, Kriketi, baseball na michezo mingine mingi ya Live na pre-match.

Previous articleMTIBWA SUGAR SIO KINYONGE YAFANYA KWELI
Next articleBACCA AMPA TANO GAMONDI