Home Sports ARSENAL NA CHELSEA NANI KUIBUKA MBABE LEO?

ARSENAL NA CHELSEA NANI KUIBUKA MBABE LEO?

Uingereza kutapigwa mechi kubwa na ya kibabe kabisa katika ya miamba miwili ya soka kutoka jiji la London klabu ya Arsenal watacheza dhidi ya Chelsea.

Mchezo huu ni mchezo wa Derby kwani vilabu vyote vinatoka katika jiji la London na timu zinazokutana pia ni kubwa, Hivo inatosha kuonesha mchezo wa leo utakaokwenda kupigwa katika dimba la Emirates una hadhi ya aina gani.

Mchezo huu ni muhimu kwa vilabu vyote viwili kwani klabu ya Arsenal ambao ni vinara mpaka sasa wa ligi kuu ya Uingereza wao watahitaji kushinda mchezo huu kwa kiwango kikubwa ili kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa huo msimu huu.

Chelsea wao pia mchezo utakua muhimu sana kwao kwani wakifanikiwa kushinda mchezo huu watakua na matumaini ya kucheza michuano ya ulaya mwakani,Ambapo kama watakosa ligi ya mabingwa basi watapata Uefa Europa league au Uefa Conference League.

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye michuano mbalimbali barani ulaya na duniani kote. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Timu hizi zinakutana ambapo Arsenal atakua na kumbukumbu ya kusimamishwa na Chelsea wakiwa na fomu nzuri kabisa na kulazimishwa sare ya mabao mawili kwa mawili, Hivo mchezo wa leo ndio utaamua ni nani mbabe wa mwenzake katika msimu huu wa 2023/2024.

Previous articleJKT TANZANIA V YANGA KUPANGIWA TAREHE
Next articleFEI TOTO AFICHUA JAMBO HUKO