CHAMA cha Mapinduzi CCM kimelitaka Shirika la Umeme nchini TANESCO lijitafakari kwakuwa si kila sababu za TANESCO kuhusu kukatika kwa umeme nchini zina mashiko ila nyingine ni uzembe.
–
Hayo yameelezwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Paul Makonda katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
–
Amesema chama hicho hakifurahii katika katika ya umeme hivyo kupelekea uvunjifu wa bodi ya utendaji ya TANESCO mara kadhaa.
–
“Ukiona Rais anavunja bodi, ujue amefikia kusema hii haivumiliki,” amesema katibu huyo.
–
“Je, mnaona mnafaa kumuwakilisha Dk. Samia?.” Ameuliza Makonda.
–
Aidha, Makonda ameitaka TANESCO kuhakikisha ahadi yake ya kuwasha kinu cha kufua umeme katika Bwawa la Nyerere JNHPP mnamo Januari, 2024 ili kupunguza makali ya umeme nchini.