Home Sports MBABE WA YANGA KUIBUKIA MTIBWA SUGAR

MBABE WA YANGA KUIBUKIA MTIBWA SUGAR

ZUBER Katwila, aliyekuwa kwenye benchi Uwanja wa Highland Estate ubao uliposoma Ihefu 2-1 Yanga anatajwa kuwa katikà hesabu za mabosi wake wa zamani Mtibwa Sugar.

Baada ya kupewa mkono wa asante ndani ya Ihefu Oktoba 14 2023 Nyerere Day kocha huyo alikuwa anatajwa kuibukia ndani ya Singida Fountain Gate.

Dili lake la kuibukia hapo lilikwama baada ya mabosi wa Singida Fountain Gate kumpa kibarua kocha mpra raia wa Brazil Ricardo Ferreira ambaye ameshaanza majukumu yake.

Mtibwa Sugar haijawa katika mwendo mzuri ñdani ya msimu wa 2023/24 kwenye mechi tano haijaambulia ushindi zaidi ya sare mbili zilizoipa pointi mbili.

Katwila amepewa mkono wa Asante ñdani ya Ihefu hivyo muda wowote kuanzia sasa atakuwa katika changamoto mpya ikiwa makubaliano yatakuwa sawa pande zote

Previous articleSUALA LA KUBEBA MATOKEO MFUKONI LISIPEWA NAFASI
Next articleMASTAA SIMBA WAJAZWA NOTI MAPEMAAA