CLATOUS Chama kiungo mshambuliaji ndani ya kikosi cha Simba ameweka wazi kuwa ikiwa atakosa tuzo ya kiungo bora ndani ya Ligi Kuu Bara kisha wakachukua nyota wengine anaocheza nao ndani ya Simba kwake itakuwa furaha.
Simba imegotea nafasi ya pili na vinara ni watani zao wa jadi Yanga chini ya Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.
Yanga pia ni mabingwa wa msimu wa 2022/23 baada ya kufikisha pointi 74.