Home Sports SINGINDA WAPOTEZA,YANGA UBINGWA WANUKIA

SINGINDA WAPOTEZA,YANGA UBINGWA WANUKIA

IKIWA Uwanja wa Liti, Singida Big Stars imeshuhudia pointi tatu zikisepa mazima kuelekea kwa wapinzani wao Yanga.

Ubao umesoma Singida Big Stars 0-2 Yanga huku kazi ikimalizwa kipindi cha kwanza.

Mabao ya Aziz KI na Clement Mzize yameipa Yanga pointi tatu na wanafikisha pointi 71 kibindoni wakielekea kutetea ubingwa wa ligi.

Mchezo ujao dhidi ya Dodoma Jiji utatoa picha kamili kw mabingwa hao watetezi kusepa na taji hilo kwa mara nyingine tena.

Ni dakika ya 15 Aziz KI alipachika bao akiwa nje ya 18 na Mzize alipachika bao hilo dakika 20 akitumia pasi ya Jesus Moloko.

Previous articleZAMA ZA AZAM FC NA SIMBA ZILIKUWA NGUMU
Next articleBADO TATU YANGA BINGWA, BOSI SIMBA,BALEKE WAPISHANA KAULI