NJE ndani TP Mazembe kaacha pointi tatutatu mbele ya Yanga walipokutana kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi wote wakiwa kundi D.
Yanga wamekamilisha mechi ya sita wakiwa wanaongoza kundi na kibindoni wana pointi 13, hapa tunakuletea kazi ilivyokuwa Uwanja wa TP Mazembe:-
Lenny Junior
Kipa huyu aliokoa hatari dakika ya 6,14,15 alipiga faulo dakika ya 46 huku akitunguliwa bao moja dakika ya 63.
Christian Kwame
Nyota huyu alikuwa kwenye kazi ngumu katika kutimiza majukumu yake dakika ya 28,43,29 alimwaga krosi kuelekea lango la Yanga.
Luzoro Sita
Ni dakika ya 11,12 alimwaga krosi alipiga faulo dakika ya 38 na dakika ya 47 shuti lake lililenga lango.
Kouame
Nahodha Christina Kouame ni shuhuda wa timu hiyo ikiambulia pointi tatu kwenye mechi sita huku ikifungwa nje ndani na Yanga yeye akiwa na kitambaa cha unahodha.
Joel Beya
Alimwaga krosi dakika ya 10,66 alicheza faulo dakika ya 32 akaonyeshwa kadi ya njano, alipiga shuti ambalo halikulenga lango dakika ya 61 na dakika ya 12 na 61 alipiga mashuti ambayo yalilenga lango.
Alex Ngonga
Bao pekee ambalo waliwafunga Yanga Uwanja wa Mkapa lilifungwa na mwamba huyu dakika ya 80. Shuguli yake kwenye mchezo wa Uwanja wa TP Mazembe ilikuwa nzito kwelikweli.
Alikutwa kwenye mtego wa kuotea dakika ya 7 alicheza faulo dakika ya 40,48 82 alionyeshwa kadi ya njano kama ilivyokuwa dakika ya 88 na kuonyeshwa kadi nyekundu, alirusha dakika ya 8 alipiga shuti ambalo halikulenga lango dakika ya 79.
Metacha Mnata
Aliokoa hatari dakika ya kwanza kisha kazi iliendelea dakika ya 6,12,14,17,42,43,45,47,60,61,71,89,90 alipiga faulo dakika ya 22.
Moloko
Jesus Moloko alipiga krosi dakika ya 6,7,40,63.
Mudathir Yahya
Muda alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 52, alipiga shuti lililolenga lango dakika ya 6 lile ambalo halikulenga lango ilikuwa dakika ya 18 huku akimwaga krosi dakika ya 31.
Aliyeyusha dakika 54 nafasi yake ilichukuliwa na Farid Mussa ambaye alifunga dakika ya 63.
Musonda
Kennedy Musonda alipiga krosi dakika ya 6,16,45 alipiga faulo dakika ya 45 aliyeyusha dakika 80 aliingia Clemnt Mzinze.
Bacca
Ibrahim Abdalah, ‘Bacca’ aliokoa hatari dakika ya 10,28,31,42,43,45,46,49 alipiga krosi dakika ya 6,17 alicheza faulo dakika ya 21 alichezewa faulo dakika ya 26,32.
Mayele
Fiston Mayele alichezewa faulo dakika ya 82,88 alipiga krosi dakika ya 7,43 alicheza faulo dakika ya 40.
Lomalisa
Joyce Lomalisa alipiga krosi dakika ya 7,29,45,63 alipiga faulo dakika ya 11,51 aliokoa dakika ya 27.
Bangala
Yannick Bangala aliokoa hatari dakika ya 12,38,40,44 alichezewa faulo dakika ya 19,31,40,48.
Bakari Mwamnyeto
Aliokoa hatari dakika ya 14,16,21,31,31,53,58.
Salim Aboubhakari
Sure Boy alimwaga krosi dakika ya 14,19,45 alicheza faulo dakika ya 39,46 aliyeyusha dakika 65 akaingia Zawad Mauya.
Job
Dickson Job aliokoa hatari dakika ya 25,39,46,49,71 alionyeshwa kadi ya njano dakika ya 82 alichezewa faulo dakika ya 71.