YANGA YAITUNGUA TP MAZEMBE NJE NDANI

TP Mazembe wametunguliwa mabao 4-1 dhidi ya Yanga wawakikilishi wa Tanzania,Kombe la Shirikisho Afrika.

Mchezo wa kwanza Uwanja wa Mkapa ubao ulisoma Yanga 3-1 TP Mazembe.

Mchezo wa pili Uwanja wa TP Mazembe ubao umesoma TP Mazembe 0-1 Yanga ikiwa ni hatua ya makundi.

Mtupiaji ugenini ni Farid Mussa dakika ya 63 na kuifanya Yanga kufikisha pointi 13 ikiwa namba moja katika kundi.

Katika kundi D Yanga inaongoza ikiwa na pointi 13 mchezo wa mwisho unaosubiriwa katika kundi hilo ni kati ya US Monastir iliyo na pointi 10 ikiwa nafasi ya pili dhidi ya Real Bamako ambao utachezwa usiku wa saa 5.