WACHEZAJI wa Geita Gold chini ya Kocha Mkuu Fred Felix ‘Minziro’ wanaendelea na maandalizi kuelekea mchezo wao wa hatua ya robo fainali Azam Sports Federation.
Geita Gold watavaana na Yanga Aprili 8, 2023 katika dimba la Azam Complex Chamazi.
Ikumbukwe kwamba mabingwa watetezi wa taji hilo ni Yanga walioshinda dhidi ya Coastal Union.