KIUNGO wa kazi ngumu ndani ya kikosi cha Simba, Mzamiru Yassin ni habari nyingine eneo la kati kutokana na kuimarika kwenye kila mchezo ambao ataanza.
Nyota huyo kwenye mchezo dhidi ya Singida Big Stars alikuwa na majukumu matatu, kupoka mipira kwa wapinzani, kulinda na kupeleka mashambulizi kwenye lango la wapinzani.
Asilimia 80 ya mipira aliyokuwa anapiga ilikuwa inafika kwa walengwa husika na kutokana na kazi ngumu aliyofanya alichezewa faulo dakika ya 19 na 37 na aliyeyusha dakika zote 90 bila kuonyeshwa kadi ya njano.
Kwenye ligi kacheza mechi 8 kayeyusha dakika 526, kafunga bao moja na katoa pasi moja ya bao msimu wa 2022/23 ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu wa Simba, Juma Mgunda.
SAN SEBASTIÁN, 17/12/2023.- El delantero nigeriano de la Real Sociedad Sadiq Umar (c) disputa un balón con el defensa hispano marroquí del Betis Chadi Riad (d) durante el encuentro entre Real Sociedad y Betis correspondiente a la jornada 17 de LaLiga Santander, este domingo en el Reale Arena de San Sebastián. EFE/ Javier Etxezarreta