>

SIRI ZA WAPINZANI WA YANGA ZAVUJISHWA

KOCHA Mkuu wa Kipanga FC, Hassani Kitimbe amewaondoa hofu Yanga kwa kuwaambia wana nafasi ya kufuzu makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuwafunga wapinzani wao, Club Africain ya nchini Tunisia. Timu hizo zitavaana katika mchezo wa Play-Off wa Kombe la Shirikisho keshokutwa Jumatano baada ya ule wa awali kutoka suluhu kwenye Uwanja wa Mkapa,…

Read More

MNIGERIA WA SIMBA AMPA NGUVU MGUNDA

JUMA Mgunda, Kocha Mkuu wa Simba ameweka wazi kuwa kazi ambayo anaifanya Victor Ackpan raia wa Nigeria kwenye kikosi hicho siyo ya kubezwa itaonyesha matokeo hivi karibuni. Nyota huyo hakuwa chaguo la kwanza la Mgunda kwenye mechi za hivi karibuni na alianzia benchi wakati ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Simba 5-0 Mtibwa Sugar.  Mgunda…

Read More

MADRID NA LIVER FAINALI YAO IMEBUMA

MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid wataanza ugenini dhidi ya Liverpool na wababe PSG watavaana na Bayern Munich kwenye mechi za hatua ya 16 bora. Mechi za raundi hiyo zinatarajiwa kuanza kupigwa Februari 14 mpaka Machi 14, mwakani 2023 baada ya droo kuchezwa Novemba 7,2022. Liverpool na Real Madrid msimu uliopita zilikutana…

Read More

AZAM FC WANATAKA POINTI TATU

UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kuwa kwenye mechi za ligi ambazo wanacheza kwa sasa wanahitaji pointi tatu tu na mabao kutoka kwa wachezaji wao. Azam FC imetoka kuipa maumivu Simba kisha ikawatuliza Ihefu FC kwa dozi ya mwendo wa mojamoja kwa timu hizo huku mtupiaji wao akiwa ni Prince Dube.  Ofisa Habari wa Azam…

Read More

AZIZ KI KIUNGO WA YANGA ‘OUT’

AZIZ KI nyota wa Yanga atakosekana kwenye mechi tatu zinazofuata kwa timu yake hiyo msimu wa 2022/23. Sababu ya nyota huyo kukosekana kwenye mechi hizo ni maamuzi ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ambayo yametolewa kutokana na kikao cha Novemba 4,2022. Taarifa hiyo imetolewa leo Novemba 8,2022…

Read More

CHAMA AKUTANA NA RUNGU LA TFF,MECHI TATU NJE

CLATOUS Chama nyota wa Simba atakosekana kwenye mchezo dhidi ya Singida Big Stars unaotarajiwa kuchezwa kesho Novemba 9,2022 Uwanja wa Liti. Sababu ya nyota huyo kukosekana kwenye mchezo huo ni maamuzi ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania ambayo yametolewa kutokana na kikao cha Novemba 4,2022. Kamati imemfungia…

Read More

MAYELE ABAINISHA KWAMBA HAWAJAHI ILI WAFUNGWE

FISTON Mayele, mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa hawajawahi kuelekea nchini Tunisia ili wafungwe bali watajitahidi kutafuta ushindi. Kikosi cha Yanga kina kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Club Africain kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa kesho Novemba 9,2022. Tayari kikosi hicho kipo nchini Tunisia kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya…

Read More