KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco amesema kuwa watafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wanapata ushindi dhidi ya Azam FC ili kuendelea kukusanya pointi nyingi zaidi.
Simba leo Jumatano wanatatarajiwa kucheza na Azam FC katika mchezo wa mzunguko wa pili wa ligi kuu utakaofanyika katika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar.
Simba wataingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi walioupata dhidi Azam katika mchezo wa mzunguko wa kwanza kwa mabao 2-1 uliofanyika katika Uwanja wa Mkapa.
Akizungumza na Championi Jumatano, Kocha Franco alisema kuwa japo mchezo ni mgumu lakini watapambana kuhakikisha kuwa wanapata matokeo ambayo yatawafanya kutoachwa pointi nyingi dhidi ya wapinzani wao, Yanga.
“Tunafahamu kuwa Azam ni timu nzuri hivyo tunatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwao hivyo mchezo hautakuwa rahisi bali utakuwa ni mgumu hivyo tunatakiwa kupambana kuhakikisha tunapata matokeo mazuri.