CHRISTINA Mwagala, Ofisa Habari wa KMC amesema kuwa ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mtibwa Sugar unawapa nguvu ya kuanza kuwasaka wapinzani wao wajao kwenye mchezo wa ligi ambao ni Ruvu Shooting wazee wa mpapaso unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mabatini,Jumatatu.