Home Sports BEACH SOCCER LEO TIMU ZATOA ZAWADI YA PASAKA

BEACH SOCCER LEO TIMU ZATOA ZAWADI YA PASAKA

LIGI ya Beach Soccer imeendelea leo katika viwanja vya Coco Beach ambapo mechi za makundi mawili A na B zilichezwa.

Ulianza mchezo wa Kundi A kati ya Ilala v PCM ambapo baada ya mchezo kukamilika ubao ulisoma Ilala 7-7 PCM na mshindi alipatikana kwa penalti na ni Ilala ilishinda penalti 5-3 PCM.

Mchezo wa kundi B ulianza ule wa Sayari dhidi Mburahati na Sayari ilipata mabao 3-4 Mburahati.

Katika mchezo wa pili wa kundi B katika Ligi ya Beach Soccer inayodhamiwani na Global Online uliwakutanisha Kijitonyama v Mshikamano FC na ulikamilika kwa Kijitonyama kushinda mabao 9-3.

Mchezo wa mwisho ulikuwa kati ya Kisa FC 2-4 Friends Ragers ambapo kwa timu ambazo zimeshinda zimetoa zawadi ya Pasaka kwa mashabiki wao.

Previous articleRUVU SHOOTING YATUMA UJUMBE HUU KWA YANGA
Next articleMUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMANNE