Home Sports ARTETA:TULIKUWA NA KILA KITU CHAKUSHINDA,SPIDI TATIZO

ARTETA:TULIKUWA NA KILA KITU CHAKUSHINDA,SPIDI TATIZO

MABAO kutoka kwa Leandro Trossard dk 28 na Enock Mwepu dk 66 yaliweza kutosha kuipa pointi tatu Brighton mbele ya Arsenal.

Ni bao la Martin Odegaard dk 89 Uwanja wa Emirates lilitosha kuwafuta machozi washika bunduki hao wanaonolewa na Kocha Mkuu, Mikel Arteta.

Arteta amesema kuwa walikuwa wana kila kitu cha kuweza kushinda lakini haikuwa hivyo.

“Tulikuwa na umiliki mzuri wa mpira na ilikuwa nzuri kwetu tulipata nafasi nyingi lakini hatukuweza kuzitumia,hatukucheza katika spidi sahihi,”.

Arteta ametoka kupoteza kwa kufungwa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace Jumatatu huku kichapo hicho kikiwapotezea matumaini ya kuwa ndani Top 4.

Previous articleYANGA WANATAKA YOTE KWA MPIGO, KUKIPIGA LEO NA GEITA
Next articleSAIDO AWASHUKURU NBC KWA TUZO