PABLO ATWAA TUZO KWA MARA YA KWANZA

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba ametwaa tuzo ya Kocha Bora ndani ya Ligi Kuu kwa mara ya kwanza baada ya kupewa dili na Simba akichukua mikoba ya Didier Gomes.

Kwa mujibu wa Kikao cha Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) kilichokaa hivi karibuni kimetoa mapendekezo ya jina la Pablo wa Simba.

Ametwaa tuzo hiyo akiwashinda Nasreddine Nabi wa Yanga na Francis Baraza wa Kagera Sugar aliongia nao fainali.

Anakuwa ni kocha wa 7 kutwaa tuzo hiyo ambayo imekuwa na ushindani mkubwa ndani ya msimu wa 2021/22.