VIDEO:KUPOTEZA KWA SIMBA MBELE YA JWANENG GALAXY KUMEWAFUNZA

JOHN Boco nahodha wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Pablo Franco ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Red Arrows unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.

Bocco amebainisha kuwa kupoteza mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa kwa kufungwa mabao 3-1 dhidi ya Jwaneng Galaxy kumewafunza hivyo wana imani kwamba watapambana kupata matokeo mbele ya Red Arrows.