BOCCO HAJATUPIA NDANI YA LIGI MECHI 14

MSHAMBULIAJI wa Simba, John Bocco hajafunga bao ndani ya ligi kwa msimu wa 2021/22 katika mechi 14 ambazo amecheza.

Ikumbukwe kwamba Bocco ni mshambuliaji na ana kibarua cha kutetea kiatu bora ambacho alitwaa baada ya kufunga mabao 16 na asisti mbili msimu wa 2020/21.

Msimu huu mambo yamekuwa magumu kwa nyota huyo mzawa ambaye amecheza mechi 14 na kuyeyusha dakika 617 uwanjani.

Kinara wa utupiaji Simba kwenye mabao 21 ambayo wamefunga ni Meddie Kagere mwenye mabao 6 na pasi moja ya bao.

Simba kwenye msimamo ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 37 huku vinara wakiwa ni Yanga wenye pointi 45.