SABA WA SIMBA WAITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA

MACHI 15,2022 leo Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania, Kim Poulsen ameita wachezaji ambao watakaoingia kambini kwa ajili ya mechi za kirafiki zilizo kwenye kalnda ya FIFA.

Kwa upande wa kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Pablo Franco ni wachezaji 7 wameitwa ambao ni pamoja na kipa namba moja wa Simba Aishi Manula.


Beki Israel Mwenda, Shomari Kapombe na  Mohamed Hussein huku kwa upande wa viungo ikiwa ni Mzamiru Yassin na Jonas Mkude na mshambuliaji ni mmoja anaitwa Kibu Denis.