Kuelekea mchezo wa CAF Champions League kati ya Yanga SC vs Silver Strikers FC unaotarajiwa kuchezwa Oktoba 18 2025, wachezaji wa Yanga SC wameanza matizi kwa maandalizi ya mwisho.
Msafara wa Yanga SC uliojumuisha wachezaji 24 uliwasili salama Malawi, Oktoba 16 2025 na kuanza kufanya mazoezi chini ya Kocha Mkuu, Romain Folz.
Mkuu wa msafara huo kwa wawakilishi wa Tanzania kwenye anga la kimataifa ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Alex Ngai ambaye yupo na timu nchini Malawi.
Haya ni maandalizi ya mwisho kwa Yanga SC kucheza mchezo wa ugenini kusaka tiketi ya kutinga hatua ya makundi kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Oktoba 18, 2025 mchezo huo unatarajiwa kuchezwa na miongoni mwa wachezaji ambao walianza mazoezi ni Clement Mzize, Dickson Job, Ibrahim Bacca.
Baada ya mchezo huo ule wa pili utakaoamua mshindi wa kutinga hatua ya makundi itakuwa ni Yanga SC vs Silver Strikers FC, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Oktoba 25, 2025.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.