KOCHA SIMBA SC FADLU DAVIDS AFICHUA HESABU KUELEKEA MSIMU MPYA

KOCHA Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids amesema kuwa wamefanya maboresho makubwa kwenye kikosi kwa kupata saini za wachezaji ambao watakuwa na kazi kupambana kwenye mashindano ambayo watashiriki.

Simba SC msimu wa 2024/25 ilishiriki Kombe la Shirikisho Afrika na kugotea hatua ya fainali ikiwa nafasi ya pili na bingwa alikuwa RS Berkane. Msimu wa 2025/26 Simba SC itapeperusha bendera kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Fadlu ameweka wazi kuwa watakuwa kwenye aina tofauti ya mashindano ambayo yanahitaji ushindani mkubwa na aina ya wachezaji waliopo watakuwa na kazi kupambania ushindi.

“Unaona kuna wachezaji ambao wamesaini kwenye kikosi. Ni aina ya wachezaji wazuri ni saini nzuri ambazo zipo kwenye kikosi. Tutakuwa kwenye mashindano tofauti msimu huu ukiachana na ligi tutakuwa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

“Aina ya ushindani kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika ni tofauti na kwenye Kombe la Shirikisho Afrika hivyo muhimu ni kuwa imara na tayari kwa ajili ya ushindani kwenye mechi zetu ambazo tutacheza.

“Kambi ambayo ipo kwa sasa ninaona tunaendelea vizuri kuna mechi ambazo tutacheza kwa ajili ya kuwa imara zaidi hivyo bado tuna muda wakufanya maandalizi zaidi.”

Miongoni mwa wachezaji wapya ambao wamesajiliwa Simba SC ni Jonathan Sowah mshambuliaji aliyekuwa Singida Black Stars, Abrahm Morice, beki wa kushoto Anthony Mligo aliyekuwa ndani ya Namungo FC.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.