HASHEEM Ibwe, Ofisa Habari wa Klabu ya Azam FC inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, ametangaza nia ya kuwania ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, (CCM)
Ibwe amesema: “Salamu kwa Vijana wenzangu. Huu ni wakati wa kusimama imara, kuchukua nafasi na kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyataka kuyaona katika jamii zetu. Maendeleo hayaji kwa kusubiri, yanajengwa na watu wenye maono, bidii, na moyo wa kujitolea. Na hakuna kikundi chenye nguvu, maarifa, na ari kubwa kama sisi vijana.
“Tuna nguvu. Tuna uwezo. Tuna wajibu. Tushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo suala la uongozi kuchora dira yetu wenyewe. Kama si sisi, ni nani? Kama si sasa, ni lini?
“Natangaza rasmi nia yangu thabiti ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi, (CCM) ya kupeperusha bendera ya chama jimbo la Mwanga, Kilimanjaro mkoa na wilaya ninayotoka.
“Tuungane kwa pamoja, tuamke, na tuijenge Tanzania mpya yenye maendeleo ya kweli yanayoanzia kwa vijana.”
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.