YANGA KUPOTEZA IMEWAUMA KWELIKWELI

ALI Kamwe, Ofisa Habari wa Yanga amesema kuwa kupoteza mchezo wa kwanza ndani ya Ligi Kuu Bara kumewapa maumivu kwa kuwa wamesemwa mpaka na mama.

Ikumbukwe kwamba msimu wa 2024/25 Yanga ilicheza mechi 8 haikupoteza ilishinda kwenye mechi zilizo ndani ya tatu bora kwa kuifunga Simba 0-1 Yanga, Singida Black Stars 0-1 Yanga.
Ni Novemba 2 2024 ubao wa Uwanja wa Azam Complex baada ya dakika 90 ubao ukasoma Yanga 0-1 Azam FC mtupiaji akiwa ni Sillah dakika ya 33 kwenye mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa.
Mara baada ya Yanga kupoteza Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alituma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii kwa kuandika namna: “Hongereni Azam kwa ushindi dhidi ya Yanga katika mchezo wenu wa Ligi Kuu.
Pamoja na Klabu nyingine zinazoshiriki Ligi Kuu, mnaendelea kutupa Watanzania burudani kupitia soka huku Taifa likiendelea kuchapa kazi kwa amani, umoja na utulivu. Nawatakia kila la kheri.
Kamwe akaandika namna hii: “Leo tumesimangwa hadi na Mama, imeniuma sana.”

Yanga kwenye msimamo ni namba moja baada ya kucheza mechi 9 wamekusanya pointi 24 wanafuatiwa na Sigida Black Stars ni namba mbili pointi 23 baada ya kucheza mechi 10 nafasi ya tatu ni Simba yenye pointi 22 baada ya kucheza mechi 9.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM.