MATAJIRI wa Dar, Azam FC wanakibarua cha kusaka pointi tatu ndani ya uwanja ambapo Oktoba wanamechi tatu zenye dakika 9 zinazosakwa na wao pamoja na wapinzani wao pia wanazihitaji pointi hizo tatu muhimu.
Tayari Mzizima Dabi ya Azam FC v Simba mzunguko wa kwanza ulikamilika kwa ubao wa Uwanja wa New Amaan Complex kusoma Azam FC 0-2 Simba.
Hizi hapa ni mechi tatu za Azam FC ndani ya Oktoba:-
Oktoba 3 2024 : Namungo v Azam FC itachezwa saa 3:00 usiku, Uwanja wa Majaliwa.
Oktoba 18 2024: Prisons v Azam FC, Uwanja wa Sokoine, saa 10:00 jioni.
Azam FC v Ken Gold, saa 1:00 usiku itakuwa Oktoba 29 2024, Azam Complex.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi Kitabu cha Ganzi ya Maumivu, kuipata 0756 028 371.