YANGA WAMETEKA SHOW MWANZO MWISHO KIKOSI BORA

HATIMAYE usiku wa tuzo za Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2023/24 umegota mwisho na kila kitu kuwa wazi nani amekuwa nani baada ya tuzo hizo.

Kwenye kikosi bora cha msimu nyota wa Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Miguel Gamondi wametawala kila kona huku kwa upande wa Simba ambao ni watani zao wa jadi mchezaji mmoja pekee akipenya kwenye kikosi cha kwanza.

Hiki hapa kikosi bora kipo namna hii:-

Ley Matampi wa Coastal Union

Yao Kouassi wa Yanga

Mohamed Hussen wa Simba

Ibrahim Hamad wa Yanga

Dickson Job wa Yanga

Mudathir Yahya wa Yanga

Kipre Junior wa Azam FC

Maxi Nzengeli wa Yanga

Wazir Junior wa KMC

Feisal Salum wa Azam FC

Aziz Ki wa Yanga