IKIWA ni mchezo wa kwanza wa kirafiki kwa Simba imepata ushindi mbele ya El Qanah Egypt kwa mabao 3-0 chini ya Kocha Mkuu, Fadlu Davids.
Kwenye mchezo huo ni Ahoua alitupia kambani mabao mawili dakika ya 14, 16 na Okejepha alitupia bao moja ikiwa ni mchezo wa kujipima nguvu.
Bado kazi ipo kwa Simba kuelekea msimu wa 2024/25 unaotarajiwa kuanza Agosti 16 2024 ambapo mabingwa watetezi wa ligi ni Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Miguel Gamondi.