WAKIWA kwenye milima ya Uluguru, Morogoro wachezaji wa Simba wameungana na kipa mpya Ayoub Lakred.
Kipa huyo ni ingizo jipya ndani ya Simba ambapo anakuwa ni kipa wa kimataifa yeye ni raia wa Morocco na watani zao wa jadi Yanga wana kipa raia wa Mali, mdaka mishale Djigui Diarra.
Agosti 15 ilikuwa ni siku yake ya kwanza kuanza mazoezi na timu hiyo inayonolewa na Kocha Mkuu Robert Oliviera.
Agosti 17 Simba inatararajiwa kutupa kete ya kwanza katika Ligi Kuu Bara utakuwa dhidi ya Mtibwa Sugar, Uwanja wa Manungu, Morogoro.