Orodha ya wachezaji wa Yanga SC watakaokosekana mchezo vs TRA United

TRA United vs Yanga SC ni mchezo unaofuata kwenye ratiba huku mabingwa watetezi wakiwakosa nyota wanne kuelekea mchezo huo kutokana na kutokuwa fiti.

Taarifa rasmi kutoka Yanga SC imeeleza kuwa wachezaji hao watakuwa nje kwa mujibu wa ripoti ya madaktari na mchezo ambao wote wataukosa ni ule unaofuata dhidi ya TRA United.

Ibrahim Abdullah (Bacca) amepata jeraha la nyonga na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha Wiki tatu

Laurindo Dilson (Depu) amepata majeraha ya nyama za paja na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili.

Chadrack Boka amepata jeraha la enka ya mguu wa kushoto na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili.

Edmund John amepata jeraha la Bega na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili.

Mbali na wachezaji hawa wanne ikumbukwe kwamba Clement Mzize na Dickson Job nao hawatakuwa kwenye mpango wa mchezo huo kutokana na kutokuwa fiti.

***

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.