Arsenal, Paris Saint-Germain na Barcelona zote zinaonyesha nia kubwa ya kumsajili Julián Álvarez kutoka Atlético Madrid.
Kwa mujibu wa Gazeti la Michezo la Hispania, DiarioAS Arsenal tayari waliwasilisha ofa ya thamani ya euro milioni 120, lakini Atlético waliikataa wakionyesha kuwa hawapo tayari kumuachia kirahisi mshambuliaji huyo.
Sasa inasubiriwa kuona kama kutakuwa na ofa mpya au kama Atlético wataendelea kusimama imara katika msimamo wao kuhusu mustakabali wa Álvarez.
Chanzo: @DiarioAS