MANCHESTER CITY YAWAPIGA MSUMARI REIJNDERS NA AIT-NOURI KWA DAU LA EURO MILIONI 110

Kiungo Tijani Reijnders na beki wa kushoto Rayan Ait-Nouri kwa pamoja wamesaini mkataba wao wa kujiunga na Manchester City baada ya kukamilika kwa taratibu za vipimo afya afya na sasa ni wachezaji wapya wa vigogo hao wa England.

Reijnders (26) raia wa Uholanzi anatua Man City kwa dau la jumla la Euro milioni 70 akitokea AC Milan huku Ait-Nouri (24) raia wa Algeria akijiunga kwa dau la Euro milioni 40 akitokea Wolves.