JESHI LA YANGA NDANI YA DR CONGO HILI HAPA

KIKOSI cha Yanga kimewasili salama nchini DR Congo baada ya kukwea pipa Desemba 12 2024 ikiwa ni maandalizi ya mwisho kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe unaotarajiwa kuchezwa Jumamosi.

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 14 2024 utakuwa ni watatu kwa Yanga kushuka uwanjani katika anga la kimataifa.

Kwenye orodha hiyo kuna makipa watatu, viungo 12, washambuliaji watatu na mabeki 7 hivyo ni msafara wa wachezaji 25 chini ya Kocha Mkuu Sead Ramovic.

Hii hapa orodha yao:-Makipa

Diarra, Khomein, Mshery.

Mabeki
Nondo, Job, Bacca, Yao, Kibabage, Kibwana na Boka.

Viungo
Aucho, Mudathir, Mkude, Abuya, Maxi, Nkane, Sure Boy, Farid, Sheikhan, Pacome, Chama, Aziz.

Washambuliaji
Musonda, Mzize na Dube.

 

 

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM.