TABORA UNITED YATANGAZA KUACHANA NA KOCHA WAKE

Klabu ya Tabora United imetangaza kufikia makubaliano ya pande zote mbili ya kusitisha makubalino baina ya aliyekuwa kocha wake Mkuu Francis Kimanzi pamoja na msaidizi wake Yusuph Chipo kunzia leo Oktoba 21.

Taarifa ya klabu hiyo ya leo Oktoba 21, 2024 imebainisha kuwa sababu za kusitisha makubaliano hayo ni kutokana na mwenendo usioridhisha wa matokeo ambayo Timu imekuwa ikiyapata.

“Uongozi unawashukuru kwa kipindi chote walichokuwa nasi katika utumishi wao na kwamba tunawatakia kila la heri kwenye maisha yao nje ya Tabora United.” imesema taarifa hiyo.