KIKOSI cha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kitaingia kambini Agosti 28 2024 ambapo kutakuwa na mechi mbili kujiandaa na michezo ya kufuzu AFCON 2025 dhidi ya Ethiopia na Guinea itaayochezwa Septemba 4 na Septemba 14 2024.
Kaimu Mkuu wa Taifa Stars, Hemed Suleiman Morocco amesema kuwa wachezaji wanaitwa kwenye timu kulingana na mahitaji ya mechi husika pamoja na uwezo wake.
“Tunawaita wachezaji kutokana na mahitaji ya timu ambapo kulingana na mchezo husika wachezaji wanaitwa. Kuhusu Mbwana Samatta bado yupo katika timu ila hata mchezo uliopita hakuitwa nimeongea naye bado yupo kulikuwa kuna masuala fulanifulani ambayo tayari yamekwisha hivyo akihitajika ataitwa.”