IMEISHA HIYO, MWAMNYETO ANAENDELEA KUBAKIA YANGA

NAHODHA na beki wa kati wa Yanga, Bakari Mwamnyeto jana ameongeza mkataba mwengine wa miaka miwili wa kuendelea kubakia hapo.
Mwamnyeto ameongeza mkataba huo, baada ya kufikia muafaka mzuri na Uongozi wa timu hiyo, katika dau la usajili na mshahara atakaouchukua ndani ya miaka miwili atakayokuwepo.
Beki huyo alisaini mkataba huo, chini ya Mtendaji wa Klabu ya Yanga, Andre Mtine na Menejimenti ya Mwamnyeto.