WEMBLEY KUWAKA MOTO LEO NI REAL MADRID DHIDI YA BORUSSIA DORTMUND FAINALI YA UEFA

Dimba la Wembley linalopatikana nchini Uingereza katika jiji la London litawaka moto leo kwani unaenda kupigwa mchezo wa kibabe wa fainali ya ligi ya mabingwa ulaya baina ya klabu ya Real Madrid dhidi ya klabu ya Borussia Dortmund.

Klabu ya Borussia Dortmund wanarudi tena Wembley baada ya miaka 11 kupita kucheza fainali, Kwani mara ya mwisho walicheza fainali katika uwanja huo mwaka 2013 na kuambulia kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Bayern Munich.

Klabu ya Real Madrid watakua wanafukuzia taji lao la 15 kwenye michuano hiyo mikubwa kabisa barani ulaya, Huku klabu ya Borussia Dortmund wao wakiwinda taji lao la pili michuano hiyo baada ya lile waliloshinda mwaka 1997 mbele ya Juventus.

Real Madrid wao wanakwenda kucheza fainali yao ya tisa tangu mwaka 1992, Hku wakiwa wameshinda fainali zao nane zilizopita hivo ni mchezo ambao wanapewa nafasi kubwa zai ya kushinda mchezo huo kutokana na historia kua upande wao kwa kiasi kikubwa.

Suka mkeka wako kwenye mchezo huu mkali wa fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya pamoja na michezo mingine itakayopigwa wikiendi hii. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Kiuhalisia mchezo utakua mkali na wenye kuvuta hisia kali kwani vilabu vyote vina ubora mkubwa ambao umewafanya kuwepo kwenye hatua hiyo kubwa kabisa ya michuano hiyo, Huku kinachosubiriwa ni nani atatwaa taji hilo na kua bingwa mpya wa michuano hiyo.

Wikiendi hii pia ligi mbalimbali zitaendelea kama Serie ya Brazil, MLS ligi kuu nchini Marekani ambapo itapigwa michezo kadhaa kama Fluminense dhidi ya Botafogo, Inter Miami watakipiga dhidi ya St. Louis michezo yote hii unaweza kubashiri kupitia Meridianbet na kupiga mkwanja wa kutosha.