>

MASHUJAA WAPOTEZA MBELE YA SIMBA

WAKIWA na kikosi cha kazi kilichotoka kupata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Tembo FC, wameshuhudia ubao ukisoma Mashujaa 0-1 Simba.

Bao pekee la ushindi kwa Simba limefungwa na Said Ntibanzokiza ambaye alipachika bao hilo kwa mkwaju wa penalti.

Kwenye mchezo wa leo washambuliaji wa Simba walikosa umakini kwenye mchezo wa leo kufanya mashambulizi ndani ya ngome ya Mashujaa.

Fred Michael ambaye amekuja kuchukua mikoba ya Jean Baleke hakuwa na hatari ndani ya 18 na nje ya 18 jambo ambalo lilimfanya akamwe kukamilisha dakika 90 ndani ya Lake Tanganyika ukiwa ni mchezo wake wa kwanza ndani ya ligi.

Ipo wazi kwamba Simba wamecheza bila mipango kuanzia safu ya kiungo mpaka ushambuliaji ambapo hakukuwa na ubunifu ni butubutu mwanzo mwisho.

Mashujaa walikosa utulivu kusaka bao la kusawazisha kwa kuwa kipindi cha pili walifanya msako wa maana kuliandama lango la Aishi Manul.

Zuber Dabi alikuwa kwenye ubora wake katika kipindi cha pili alikosa bahati ndani ya kipindi cha pili kufunga bao na kushuhudia wakiyeyusha pointi tatu wakiwa nyumbani.