>

IHEFU WAKOMBA POINTI ZA TABORA UNITED

WAKIWA Uwanja wa Highland Estate Ihefu walikomba pointi zote tatu mazima kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tabora United.

Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa mwamba Vedastus Mwihambi alipachika mabao yote kwa Ihefu ilikuwa dakika ya 40 na dakika ya 56.

Kwenye mchezo huo uliochezwa Desemba 8 ni bao la Andy Bikoko lilikuwa lakufutia machozi dakika ya 80 huku pointi tatu zikibaki kwenye ngome ya wakulima wa mpunga, Ihefu.

Ihefu inafikisha pointi 13 nafasi ya 13 ikiwa imecheza mechi 13 wastani wa kukusanya pointi moja kila mchezo.

#iNDEPENDETDAYTANGANYIKA 62