MATOLA SELEMAN KAZINI NDANI YA SIMBA

SELEMAN Matola, kocha msaidizi wa Simba ameanza kazi ya kuwanoa wachezaji wa timu hiyo.

Novemba 8 2023 alitambulishwa kurejea ndani ya kikosi cha wakubwa baada ya kuwa katika timu ya vijana.

Anashirikiana na Kaimu Kocha Mkuu Cadena Daniel ambaye alikuwa ni kocha wa makipa akichukua kwa muda majukumu ya Roberto Oliveira raia wa Brazil.

Mchezo wa kwanza kwa benchi hilo jipya unatarajiwa kuwa Novemba 9 Uwanja wa Uhuru dhidi ya Namungo FC unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Uhuru.