>

KIUNGO WA KAZI SIMBA AREJEA NA KUANZA MATIZI

NELSON Okwa kiungo wa Simba amerejea kwenye kikosi na kuanza mazoezi na wachezaji wenzake wa timu hiyo.

Okwa ni ingizo jipya ndani ya kikosi cha Simba hajawa kwenye mwendo mzuri kwa kwa hakuwa fiti.

 Okwa alikuwa anasumbuliwa na tatizo la nyonga kwa mujibu wa Kocha Mkuu wa Simba Juma Mgunda.

Hakuwa kwenye mchezo uiopita wa Simba dhidi ya Coastal Union, uliochezwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga na timu hiyo kushinda mabao 0-3.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally amesema kuwa nyota huyo kwa sasa yupo fiti baada ya kupata matibabu.