>

LIVERPOOL WAMECHANA MKEKA

TAIWO Awoniyi amezima furaha ya mashabiki wa Liverpool na kuwafanya Nottm Forest kubaki na pointi tatu wakiwa nyumbani.

Kwenye mchezo wa Ligi Kuu England, bao la ushindi limefungwa dakika ya 55kipindi cha pili jitihada za Liverpool kusaka usawa na ushindi zikakutana na uimara wa kipa wa wapinzani wao.

Ni mashuti 10 Nottm walipiga na 7 yalilenga lango kama Liverpool ambao walipiga jumla ya mashuti 15.

Pointi zao ni 9 wakiwa nafasi ya 19 huku Liverpool wakiwa nafasi ya 7 pointi 16.