CHELSEA WAICHAPA CRYSTAL PALACE USIKU

USIKU kabisa Chelsea wakiwa ugenini wamepeleka maumivu kwa Crystal Palace kupitia kwa Conor Gallagger dakika ya 90.

Bao hilo lilifanya ubao wa Uwanja wa Selhurst Park kusoma, Crystal Palace 1-2 Chelsea.

Bao la mapema kwa Crystal Palace lilijazwa kimiani na Odsonne Edouard dakika ya 9 liliwekwa usawa na Pierre Emerick Aubameyang dakika ya 38.

Chelsea inafikisha pointi 13 nafasi ya tano na Crystal nafasi ya 17 na pointi ni 6 kibindoni.