RATIBA LIGI KUU BARA

LIGI Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo Juni 18, ambapo timu mbili zitakuwa na kazi ya kusaka pointi tatu muhimu.

Ni Geita Gold itawakaribisha Biashara United katika Uwanja wa Nyankumbu.

Geita Gold ipo nafasi ya 4 ikiwa na pointi 39 inakutana na Biashara United iliyo nafasi ya 15 na pointi 25.

Pia mchezo mwingine ni ule dhidi ya Kagera Sugar iliyo nafasi ya 7 na pointi 34 itamenyana na Dodoma Jiji iliyo nafasi ya 12 na pointi 31