Home Sports MKOMBOZI WA SIMBA KWENYE MAJUKUMU MAZITO

MKOMBOZI WA SIMBA KWENYE MAJUKUMU MAZITO

SIMBA iliyo chini ya Kocha Msaidizi Seleman Matola imemtambulisha rasmi nyota Moses Phiri ambaye alikuwa anakipiga ndani ya Klabu ya Zanaco.

Huu unakuwa ni usajili wa kwanza kwa Simba ambao msimu huu wamepoteza kila taji amalo lilikuwa mkononi mwao.

Ni dili la miaka miwili nyota huyo amepewa ambapo anamajukumu ya kuweza kufanya kazi ya kutibu tatizo la ubutu wa ushambuliaji ambalo linaitesa Simba msimu huu wa 2021/22.

Nyota mwingine ambaye anatajwa kuweza kutua ndani ya Simba ni Aziz KI ambaye huyu dili lake ni gumu kwa kuwa Yanga wao wameonesha nia ya kumpata nyota huyo.

Na kuna asilimia kubwa kwamba nyota huyo anaweza kutambulishwa Yanga.

Previous articleYANGA:UBINGWA ASILIMIA 99
Next articleYANGA YATWAA UBINGWA WA 28 BONGO