BEKI YANGA AONGEZA DILI JIPYA

RASMI beki kisiki wa Yanga ambaye ni nahodha pia Bakari Nondo Mwamnyeto ameongeza kandarasi ya miaka miwili kuendelea kuitumikia timu hiyo.

Mkataba wa nyota huyo ambaye aliibuka hapo akitokea kikosi cha Coastal Union ulikuwa unatarajiwa kufika tamati mwishoni mwa msimu wa 2021/22.

Miongoni mwa timu ambazo zilikuwa zinatajwa kuwania saini yake ni pamoja na timu kutoka Uarabuni na nyingine ni za hapa Bongo.

Hivyo kuongeza kwake dili kutawafanya mashabiki wa Yanga kuzidi kuona huduma ya beki huyo wa kazi chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.